Ujumbe kutoka kwa Tambwe kuelekea mechi na Simba



Amis Tambwe ni moja ya washambuliaji wa Yanga ambao walianza kusahaulika kutokana na kuwa majeruhi kwa muda mrefu lakini pia hata waliporejea hawakuonekana kuwa sumu kwa mabeki wa timu pinzani.
Lakini Juzi kati Jumapili Yanga ikicheza na Singida United Amis Tambwe alionekana kurejea kwenye makali yake kutokana na kufunga mabao mawili Yanga ikiifunga Singida bao 2 kwa 0.
Baada ya Kurejea kwa kasi hiyo Amis Tambwe amefunguka kuwa kama kocha mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera atampa nafasi ya kucheza katika mchezo huo basi atahakikisha anafunga mabao kwa namna yoyote ile iwe kwa kichwa au kwa Miguu.

No comments:

Powered by Blogger.